inasemekana hivi sasa ardhi ni rasmali kubwa
ni kumpa mjumbe wa nyumba kumi kiasi kadhaa au kumnywesha kangara, chibuku au bia mbili tatu atie dole gumba. ukishtuka unaambiwa kwamba sirikali imeigawa sehemu yako kwa sababu umeshindwa kuihudumia. na huna pa kwenda. kwani kila utakapokwenda ni mizunguko mizinguo tu ndiyo haiishi. pengine unayeongea naye ni shemeji yake huyo bosi aliyemuhonga mjumbe.
“njoo kesho, bosi hayupo. njoo kesho … njoo kesho.” utachoka mwenyewe. kufuatana na niliyosikia na kushuhudia, nchi ya kikwete na hawa wezi wezi wengine hivi sasa haina tofauti kubwa na za zamani. watu wasio na chao wanakwetwa
swali, je, watu waliokuwa wakiishi pale wameishia wapi? na walipata fidia ya kutosha au kuridhisha, kufuatana na walichopoteza? au ndiyo walifanyiwa kiini macho tu? na
ni kweli kuwa hali hii iko afrika nzima. kwa mafno msumbiji mawazir walikuwa akinunua mabsha makubwa na ardhi na kuiwekeza hadi hapo bei itakapopanda halafu wanauza kwa faida ya ajabu. lakini tunazungumzia rasmi bongo. nchi ambayo inajigamba kwa kuwa salama na isiyo na shida za ubaguzi na matatizo ya uhasama wa kidini. ukabila. na matatizo mengine
hii ni amri ya sirikali aua watu fulani tu wajanja wajanja waliopewa majukumu ya kuangalia mashamba na ugawaji/ uuzaji wa mashamba na viwanja? je, huu si wizi wa kimasomaso? na yote hii ni kutokana na unyonge wa wale wanaochaguliwa na kuporwa haki zao. wenye pesa sehemu zao haziguswi kamwe. sasa haki na usawa viko wapi?
navyoona mimi sirikali ingewaambia watu kuwa maeneo
mwalimu alishindwa na ujamaa wake. sababu kubwa ni kuwa watendaji wa kanuni zake walikuwa wakitenda kinyume au shingo upande. kwani walikuwa wakiona uhondo unawapita tu hivi hivi walipofananisha na wenzao wa
kweli kuna majumba ya maghorofa marefu ya chuma na vioo na watu wengi wana tv (za hali duni), magari ya kupendeza na kuvutia (kupendeza hakumaanishi ubora). kwa wengine, wengi wasioelewa na wenye akili finyu, haya ni maendeleao. lakini maendeleo hasa ni watu na siyo vitu.
swali, ukabaji huu utakaposhindwa, au wananchi wakichoka kuonewa na kunyanyaswa, sulushisho litakuwa nini?
sidhani tena, na ni wazi,
walio baki alamsiki.
No comments:
Post a Comment